Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MWALIMU wa Shule ya Msingi Katani wilayani Nkasi, Rukwa Ringtone
Rayson (36) amehukumiwa kwenda jela miaka miwili au kulipa faini ya sh
100,000 kwa makosa ya kufumaniwa na kumjeruhi mume wa mwanamke
aliyekuwa naye.
Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa
Mahakama ya Wilaya ya Nkasi, Ramadhani Rugemalila, Mwendesha Mashitaka
Hamimu Gwelo, alisema mtuhumiwa huyo alifumaniwa na mke wa Richard
Feruzi (33) aitwaye Beata Sangu (31).
Pamoja na hukumu hiyo, mtuhumiwa alitakiwa kulipa faini ya sh 300,000
kutokana na majeruhi aliyomsababishia Feruzi na mdogo wake Stanslaus
Feruzi waliokuwepo siku ya tukio.
Chanzo;Tanzania daima
0 comments:
Post a Comment