KIWANJA CHA NDEGE SUMBAWANGA CHAFIKIA ASILIMIA SITINI YA UJENZI.

Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga umefikia asilimia sitini ya utekelezaji wake. Taarifa hiyo imetolewa mbele waandishi wa habari leo Machi 26, 2025 na Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Rukwa, Mhandisi Joseph Jimonge.Ameeleza kuwa mradi huo unaogharimu bilioni 60 unatarajia kukamilika Juni 2025.Mhandisi Jimonge ameeleza kuwa ujenzi wa kiwanja hicho unalenga kuimarisha uchumi kwa kuimarisha sekta ya usafiri na usafirishaji Mkoani hapa na kuwa kichocheo cha kufunguka kwa fursa mpya za kibiashara."Kiwanja cha ndege cha Sumbawanga kitaleta mabadiliko makubwa katika uchumi wa Mkoa wa Rukwa. Zaidi ya abiria 150,000...

RUKWA KUPATA UMEME WA UHAKIKA : JIWE LA MSINGI LAWEKWA KATIKA MRADI MKUBWA

Na Khadija DalasiaMkoa wa Rukwa unatarajia kupata umeme wa uhakika baada ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dr.Dotto Mashaka Biteko, kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa kusafirisha umeme wa Kilovoti 400 kutoka Mkoani Iringa hadi Sumbawanga na kuunganisha Tanzania na Zambia ambao utaunganisha Bara la Afrika kutoka Afrika Kusini hadi Ethiopia.Akizungumza katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi mradi huo wa TAZA iliyofanyika leo, Julai 29, 2024, katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, Kata ya Malangali, Mheshimiwa Dr. Biteko amesema kuwa Serikali imekuwa ikitumia takribani shilingi bilioni 15 kila Mwaka kununua umeme...

KAMATI YA SIASA YA MKOA WA RUKWA YATAKA USIMAMIZI MADHUBUTI MIRADI YA UJENZI.

Na Khadija Dalasia Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Rukwa ikiongozwa na Mheshimiwa Mwenyekti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa, Hajjat Silafu Jumbe Maufi imewataka Wakurugenzi wa Halmashauri Mkoani Rukwa kusimamia vyema miradi ya ujenzi katika maeneo yao.Kamati hiyo imegiza hayo leo Julai 25, 2024 ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake ya ukaguzi wa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya 2020-2025 katika Halmashauri za Mkoa wa Rukwa.Mheshimiwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa amesema kuwa ili kupata miradi yenye ubora unaolingana na thamani ya fedha zinazotolewa na Serikali, Wakurugenzi wanatakiwa kuisimamia kwa karibu ikiwemo kuwawezesha wahandisi kuisimamia kwa...

CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA RUKWA CHARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA MANISPAA YA SUMBAWANGA

Kamati ya Siasa Mkoa wa Rukwa ikiongozwa na Hajjat Silafu Jumbe Maufi, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Rukwa imeridhishwa na ubora wa miradi inayotekelezwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga.Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Rukwa imeanza ziara ya siku nne katika Halmashauri za Mkoa wa Rukwa ikikagua  utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2020 -2025 katika Mkoa wa Rukwa kuanzia tarehe 24 Julai hadi tarehe 27 Julai 2024.Wajumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Rukwa wamekagua utekelezaji wa miradi  8 yenye thamani ya shilingi Bilioni 3.1 katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga. Miradi iliyokaguliwa...

WAKULIMA NKASI WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA UMWAGILIAJI KUINUA KIPATO.

Na Khadija Dalasia,Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Charles Makongoro Nyerere amewataka wananchi  wa Kata za Kirando, Kipili na Kitete Wilayani Nkasi kutumia fursa ya mradi wa umwagiliaji unaojengwa katika Kata hizo kuinua kipato chao.Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo Julai 23, 2024 aliposhuhudia utiaji saini na makabidhiano ya mradi wa skimu ya umwagiliaji ya Lwafi - Katongolo kati ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Mkandarasi M/S Halem Construction Company Limited. Zoezi la makabidhiano ya mradi huo wenye thamani ya shilingi Bilioni 20.9 utakaotekelezwa kuanzia Julai 2024 hadi Julai 2026 limefanyika katika Kijiji cha Katongolo wilayani...

Matukio mbalimbali kwenye Mkutano wa hadhara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan uliofanyika katika uwanja wa Nelson Mandela Sumbawanga Mkoani Rukwa

Matukio mbalimbali kwenye Mkutano wa hadhara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan uliofanyika katika uwanja wa Nelson Mandela Sumbawanga Mkoani Ru...

Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aweka jiwe la Msingi la ujenzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya, Kampasi ya Rukwa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuweka jiwe la Msingi la ujenzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya, Kampasi ya Rukwa kwenye hafla iliyofanyika katika Kijiji cha Kianda Mkoani Rukwa tarehe 17 Julai, 2024.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kianda mara baada ya kuweka jiwe la Msingi ujenzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya, Kampasi ya Rukwa tarehe 17 Julai, 2024. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia...
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa