Na Walter Mguluchuma
Nkasi
HALI
ya Taharuki na hofu imezuka katika kijiji cha Katani kata ya Nkandasi
wilayani Nkasi mkoani Rukwa na kupelekea waombolezaji kutimua mbio na
kuacha jeneza lenye mwili wa marehemu baada ya mvua kubwa kuanzakunyesha
na kubomoa nyumba za wakazi wa kijiji hicho.
Tukio hilo lilitokea Juzi
majira ya saa 6 mchana mara baada ya kuanza kunyesha mvua kubwa
zilizoambatana na radi na upepo mkali ulioezua baadhi ya nyumba za
wanachi hao ambao walikuwa wakiomboleza msiba wa mwananchi mwenzao
aliyefaniki baada ya kuugua siku chache zilizopita.
Akizungumza na gazeti hili
mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Kaungo, Robert Kanoni alisema
kuwa wakiwa wanaelekea kufanya maziko ya marehemu Dismas Kanoni
aliyefari Jana, ghafla ilianza kunyesha mvua kubwa ikiambatana na radi
na upepo mkali hali iliyosababisha baadhi ya waombolezaji kutimua mbio
na kurejea majumbani kutokana na hofu iliyoibuka kufuatia tukio hilo.
Baadhi ya wananchi
walivumilia nakurejea na jeneza lililokuwa na mwili wa marehemu nyumbani
na kuahilisha maziko kwamuda ili kupisha hali hiyo uweze kutulia na
walikwenda kuzika baadaye katika makaburi yaliyopo kijijini hapo.
Alisema kuwa tukio hilo
limezua hisia za kishirikina kwa wananchi wa kijiji hicho kwani miezi
miwili iliyopita baba yake na marehemu huyo alifariki baada ya kugongwa
na gari la kampuni ya ujenzi wa barabara na walipofanya maziko siku iliyofuata walikuta ngozi ya kondoo juu ya kaburi la marehemu kitendo kilicho washangaza wakazi hao.
Kanoni alisema kuwa kutokana
na mvua hiyo nyumba zipatazo 10 zimebomoka kabisa na zinatakiwa
kujengwa upya huku nyumba nyingine Saba, zikiwa zimeezuliwa paa na
kuwaacha wakazi wake wakiwa hawana sehemu ya kukaa licha ya kuwa
wamepata hifadhi na misaada ya kibinaadamu kwa wenzao.
Naye Peter Kalale mkazi wa
kijiji hicho akizungumzia tukio hilo alisema kuwa mara kwa mara kijiji
hicho kimekuwa kikikumbwa na dhoruba pindi mvua zinaponyesha kwakua
kimepitiwa na mkondo wa upepo mkali ambao unasababisha hali hiyo.
Alisema changamoto iliyopo
ni tabia ya wananchi kukata miti kwaajili ya mashamba na hivyo
kusababisha pepo zinapovuma hazikuti kizuizi chochote na hivyo imekuwa
sababu ya kuezuliwa nyumba zao na hata kubomoka kabisa.
Kwaupande wake mwenyekiti wa
kamati ya maafa ya wilaya hiyo ambaye ni mkuu wa wilaya hiyo Said
Mtanda ilikiri kutokea kwa tukio hilo na kutoa wito kwa wananchi kujenga
makazi bora kwani miongoni mwa nyumba hizo zipo ambazo zimeezekwa kwa
nyasi.
Alisema kuwa sera ya
serikali ya awamu ya tano ni kuwahimiza wananchi wajenge nyumba bora na
zakisasa ili waweze kuepuka majanga yanayotokana na tabia nchi kwani
bila kufanya hivyo wananchi wataendelea kupata hasara.
0 comments:
Post a Comment