Home » » MVUA KUBWA YASABABISHA WATU KUKIMBIA JENEZA

MVUA KUBWA YASABABISHA WATU KUKIMBIA JENEZA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
 
Na   Walter  Mguluchuma
Nkasi
HALI ya Taharuki na hofu imezuka katika kijiji cha Katani kata ya Nkandasi wilayani Nkasi mkoani Rukwa na kupelekea waombolezaji kutimua mbio na kuacha jeneza lenye mwili wa marehemu baada ya mvua kubwa kuanzakunyesha na kubomoa nyumba za wakazi wa kijiji hicho.

Tukio hilo lilitokea Juzi majira ya saa 6 mchana mara baada ya kuanza kunyesha mvua kubwa zilizoambatana na radi na upepo mkali ulioezua baadhi ya nyumba za wanachi hao ambao walikuwa wakiomboleza msiba wa mwananchi mwenzao aliyefaniki baada ya kuugua siku chache zilizopita. 

Akizungumza na gazeti hili mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Kaungo, Robert Kanoni alisema kuwa wakiwa wanaelekea kufanya maziko ya marehemu Dismas Kanoni aliyefari Jana, ghafla ilianza kunyesha mvua kubwa ikiambatana na radi na upepo mkali hali iliyosababisha baadhi ya waombolezaji kutimua mbio na kurejea majumbani kutokana na hofu iliyoibuka kufuatia tukio hilo.

Baadhi ya wananchi walivumilia nakurejea na jeneza lililokuwa na mwili wa marehemu nyumbani na kuahilisha maziko kwamuda ili kupisha hali hiyo uweze kutulia na walikwenda kuzika baadaye katika makaburi yaliyopo kijijini hapo. 

Alisema kuwa tukio hilo limezua hisia za kishirikina  kwa wananchi wa kijiji hicho kwani miezi miwili iliyopita baba yake na marehemu huyo alifariki baada ya kugongwa na gari la kampuni ya ujenzi wa barabara na walipofanya maziko siku iliyofuata walikuta ngozi ya kondoo juu ya kaburi la marehemu kitendo kilicho washangaza wakazi hao.

Kanoni alisema kuwa kutokana na mvua hiyo nyumba zipatazo 10 zimebomoka kabisa na zinatakiwa kujengwa upya huku nyumba nyingine Saba,  zikiwa zimeezuliwa paa na kuwaacha wakazi wake wakiwa hawana sehemu ya kukaa licha ya kuwa wamepata hifadhi na misaada ya kibinaadamu kwa wenzao.  

Naye Peter Kalale mkazi wa kijiji hicho akizungumzia tukio hilo  alisema kuwa mara kwa mara kijiji hicho kimekuwa kikikumbwa na dhoruba pindi mvua zinaponyesha kwakua kimepitiwa na mkondo wa upepo mkali ambao unasababisha hali hiyo. 

Alisema changamoto iliyopo ni tabia ya wananchi kukata miti kwaajili ya mashamba  na hivyo kusababisha pepo zinapovuma hazikuti kizuizi chochote na hivyo imekuwa sababu ya kuezuliwa nyumba zao na hata kubomoka kabisa. 

Kwaupande wake mwenyekiti wa kamati ya maafa ya wilaya hiyo ambaye ni mkuu wa wilaya  hiyo Said Mtanda ilikiri kutokea kwa tukio hilo na kutoa wito kwa wananchi kujenga makazi bora kwani miongoni mwa nyumba  hizo zipo ambazo zimeezekwa kwa nyasi.

Alisema kuwa sera ya serikali ya awamu ya tano ni  kuwahimiza wananchi wajenge nyumba bora na zakisasa ili waweze kuepuka majanga yanayotokana na tabia nchi kwani bila kufanya hivyo wananchi wataendelea kupata hasara.


Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa