Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dk. Khalfan Haule akitoa maelezo ya kumtambulisha Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo kwa wananchi wa kijiji cha Zimba kata ya Mtowisa, Wilayani Sumbawanga. wakati walipofika kwenye kijiji hicho kuona kiwanda cha kukamulia alizeti.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (wa tatu kutoka kulia) akiuliza swali kwa mhandisi wa maji wa Wilaya Patrick Ndimbo (wa kwanza kushoto) wakati walipotembelea mradi wa maji wa kutumia umeme wa jua mji mdogo Laela Wilayani Sumbawanga wenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.8.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akishiriki kutumia ala ya kigoda kuchekecha juu ya mtungi na kuzalisha sauti inayowezesha kuleta mlio kwaajili ya kunogesha nyimbo, Ni ala ya asili inayotumiaka katika ngoma za kitamaduni za Kifipa muda mfupi kabla ya kufanya mkutano na wananchi wa mji mdogo wa Laela.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akimsalimia mmoja wa kinamama wa kikundi cha ngoma Laela Odila Maufi wakati alipokuwa akiingia katika viwanja vya shule ya Msingi Laela kwaajili ya Mkutano wa hadhara kujitambulisha kwa wananchi na kuongea nao.
Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewasifu wananchi wa kata ya
Mtowisa, Tarafa ya Mtowisa, Wilayani Sumbawanga kwa kuonyesha mshikamano
katika ujenzi wa shule ya Sekondari Vuma pamoja na ujenzi unaonendelea
wa kituo cha polisi kitakachohudumia tarafa ya mtowisa.
Tarafa
hiyo yenye kata 4 ina shule moja ya kidato cha tano na sita jambo
alilosifu Mh. Wangabo kuwa imetimiza ilani cha Chama Tawala kwa kuwa na
Shule moja ya aina hiyo kwa kila tarafa.
Amesema
kuwa ataendelea kusisitiza kauli ya serikali ya awamu ya tano ya kuwa
maendeleo hayana vyama, hivyo alisisitiza wananchi hao kutobaguana kwa
itikadi zao bali wahimizane katika kutatua changamoto na kuleta
maendeleo katika tarafa yao.
“Mmenivuti
mliponieleza kwamba mnashirikiana katika nyanja mbalimbali, kuna
majengo yale ya shule mnashirikiana na jengo hili la polisi
mnashirikiana ili kuhakikisha kwamba changamoto mbalimbali zilizopo
ndani yenu mnazitatua, hili limenifurahisha na ningependa muendelee
nalo, na umeoja na mshikamano uliopo muudumishe bila ya kujali vyama
vyenu.” Alisifu.
Ameyasema
hayo katika Mkutano wa hadhara katika Kijiji cha mtowisa, kata ya
mtowisa Wilayani Sumbawanga katika ziara yake ya siku mbili katika
Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga yenye lengo la kutembelea miradi
mbalimbali na kujitambulisha kwa wananchi.
Kwa
upande wake diwani wa Kata ya mtowisa Mh. Edgar Malini alisema kuwa
wananchi wa mtowisa hawana tabu wa kutoa ushirikiano ili kujiletea
maendeleo wenyewe isipokuwa wamekuwa na kilio cha muda mrefu kuhusu
umeme na maji.
0 comments:
Post a Comment