Na Walter Nguruchuma- Katavi yetu
MAHAKAMA ya Wilaya ya Nkasi mkoani
Rukwa imemuhukumu mkazi wa kijiji cha Mashete , Titho Solwe (20)
kutumikia kifungo cha miaka 30 jela baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la
kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 10.
Akitoa hukumu hiyo jana , Hakimu
Mfawidhi wa Mahakama hiyo ya Wilaya , Lilian Lutehangwa alisema kuwa
mahakama imeridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na
upande wa mashtaka pasipo kutia shaka yeyote kuwa mshtakiwa alitenda kosa
hilo na walasi si mtu mwingine .
Upande wa Mashtaka ulioongozwa na
Mwendesha Mashataka , Mkaguzi wa Polisi , Hamimu Gwelo uliita mashahidi
watatu mahakamani hapo . “Mahakama hii imeridhishwa na ushahidi
uliotolewa na upande wmashtaka ambao hauachi chembe yayote ya
mashaka kuwa si mtu mwingine aliyemtendea unyama mtoto huyo
bali ni huyu mshtakiwa mwenyewe” alisema akitoa hukumu hiyo .
Awali Gwelo alidai mahakamani hapo
kuwa mshtakiwa huyo alitenda uhalifu huo Juni, 19 mwaka huu katika kijiji
cha Mashete kilichopo katika Kata ya Mtenga wilayani Nkasi mkoani
hapa .
0 comments:
Post a Comment