Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma , Sumbawanga
WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), umemkabidhi Mkuu wa mkoa
wa Rukwa , Zelothe Steven madawati 256 kwa ajili ya wanafunzi wa
shule za msingi zilizopo katika wilaya tatu mkoani humo .
Akikabidhi madawati hayo, Meneja wa shamba la Msitu wa Hifadhi wa
Mbizi , Mohamed Kiangi alisema lengo la wakala huo ni kuunga mkono
juhudi na jitihada za Rais John Magufuli za kumaliza tatizo la uhaba
wa madawati katika shule za msingi na sekondari.
Kiangi alisema, madawati hayo 256 yaliyokabidhiwa ni kati ya madawati
420 yaliyopangwa kutolewa na TFS kwa mkoa huo ambapo yatagawiwa
kwa halmashauri za wilaya za Nkasi ,Sumbawanga ,Kalambo na Manispaa ya
Sumbawanga kwa utaratibu uliowekwa.
Mkuu wa Mkoa huo , Zelothe mara baada ya kupokea madawati hayo
alisema katika kutekeleza agizo la Rais Magufuli mkoa ulifanya
jitihada kubwa ambapo madawati mapya yalitengenezwa ingawa bado
kuna upungufu.
Alisema mkoa ulikuwa na mahitaji ya madawati 84,685 ambapo
yaliyotengenezwa hadi sasa ni madawati 78,072 sawa na asilimia 92.19
ambapo upungufu ukiwa ni wa madawati 6,613 ikiwa ni sawa na
asilimia 7.8 kwa shule za msingi .
Aliwataka wakurugenzi wa halmashauri hizo nne kuhakikisha
wanasimamia na kuhakikisha madawati hayo yanatunzwa ipasavyo.
Mwisho.
WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), umemkabidhi Mkuu wa mkoa
wa Rukwa , Zelothe Steven madawati 256 kwa ajili ya wanafunzi wa
shule za msingi zilizopo katika wilaya tatu mkoani humo .
Akikabidhi madawati hayo, Meneja wa shamba la Msitu wa Hifadhi wa
Mbizi , Mohamed Kiangi alisema lengo la wakala huo ni kuunga mkono
juhudi na jitihada za Rais John Magufuli za kumaliza tatizo la uhaba
wa madawati katika shule za msingi na sekondari.
Kiangi alisema, madawati hayo 256 yaliyokabidhiwa ni kati ya madawati
420 yaliyopangwa kutolewa na TFS kwa mkoa huo ambapo yatagawiwa
kwa halmashauri za wilaya za Nkasi ,Sumbawanga ,Kalambo na Manispaa ya
Sumbawanga kwa utaratibu uliowekwa.
Mkuu wa Mkoa huo , Zelothe mara baada ya kupokea madawati hayo
alisema katika kutekeleza agizo la Rais Magufuli mkoa ulifanya
jitihada kubwa ambapo madawati mapya yalitengenezwa ingawa bado
kuna upungufu.
Alisema mkoa ulikuwa na mahitaji ya madawati 84,685 ambapo
yaliyotengenezwa hadi sasa ni madawati 78,072 sawa na asilimia 92.19
ambapo upungufu ukiwa ni wa madawati 6,613 ikiwa ni sawa na
asilimia 7.8 kwa shule za msingi .
Aliwataka wakurugenzi wa halmashauri hizo nne kuhakikisha
wanasimamia na kuhakikisha madawati hayo yanatunzwa ipasavyo.
Mwisho.
0 comments:
Post a Comment