MKUU wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Steven ameamuru watoto wa kiume wenye
umri mkubwa wanaoishi mitaani mjini Sumbawanga, wacharazwe viboko
mahakamani ili warudi na kuishi na familia zao.
Aidha, ameamuru wazazi na walezi wa watoto hao, wasakwe popote walipo
na washtakiwe kwa kuwatelekeza watoto wao na kusababisha waishi
mitaani.
Zelothe alitoa maagizo hayo katika Kikao cha 30 cha Kamati ya Ushauri
ya Mkoa wa Rukwa (RCC) mwishoni mwa wiki mjini hapa, akiunga mkono
ushauri alioutoa Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, Dk Halfani Haule.
“Hii sasa imekuwa ni kero kubwa, zipo taarifa kuwa watoto hao wana wazazi wao ….
Watoto hawa sasa wamekuwa watukutu mitaani, kwa wale wenye umri
mkubwa wasakwe , wakamatwe wafikishwe mahakamani na wapewe adhabu ya
kucharazwa viboko kisha warejeshwe kwa wazazi wao.
“Kwa wazazi wenye watoto hawa nao wasakwe , wakamatwe na kufikishwa
mahakamani ili iwe fundisho kwa wazazi wenye tabia isiyokubalika ya
kuwatelekeza watoto wao na kusababisha waishi mitaani mjini hapa,”
alisisitiza Zelothe.
Dk Haule alishauri kuwa watoto 16 wanaoishi mitaani mjini humo, ambao
wana umri mkubwa waliokamatwa hivi karibuni katika msako, waadhibiwe
kwa kucharazwa viboko mahakamani kisha warejeshwe kwenye familia zao.
“Watoto 231 wote wavulana wamebainika kuwa wanaishi mitaani katika
Mji wa Sumbawanga na umri tofauti katika msako wa hivi karibuni
uliofanyika mjini hapa watoto 40 wamekamatwa na kupelekwa kuishi kwenye
nyumba ya malezi ya Bethania, inayolea watoto wanaoishi katika mazingira
magumu ….
Katika msako huo walikamatwa watoto 16 ambao wao wana umri mkubwa
nashauri wacharazwe viboko mahakamani ili waweze kurudi kwenye familia
zao,” alisema.
CHANZO GAZETI LAHABARI LEO
0 comments:
Post a Comment