Home » » JKT yazuia madawati ya majimbo mawili

JKT yazuia madawati ya majimbo mawili

Katibu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Job Masima
WIZARA ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), imezuia majimbo mawili ya Nkasi Kaskazini na Nkasi Kusini mkoani Rukwa kupewa madawati 1,074 kutokana na kushindwa kuyachukua kwa muda uliopangwa. Aidha, imewataka wafanyakazi wa wizara hiyo kuwa tayari na safari ya kuhamia Dodoma ifikapo Novemba 30.
Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Job Masima, majimbo 18 yaliyokuwa hayajachukua madawati yao yalipewa siku saba yafanye hivyo lakini hayo mawili hayakutekeleza agizo hilo lililotolewa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Tifa, Dk Hussen Mwinyi.
“Muda wa kuchukua madawati umeisha juzi, napenda kuyapongeza majimbo 16 yaliyoitikia wito na kuchukua jumla ya madawati 8,592. Pia Wizara imesikitishwa na majimbo mawili yaliyoshindwa kufuata madawati yao,” alisema.
Madawati hayo ni miongoni mwa yaliyotengenezwa na JKT pamoja na Magereza nchini baada ya kupewa zabuni na Bunge la Tanzania kutokana na Sh bilioni sita ambazo chombo hicho kilizirejesha serikalini na Rais John Magufuli kuagiza zitumike kutengeneza madawati kwa shule nchini. Kuhusu kuhamia Dodoma, taarifa hiyo iliwataka wafanyakazi waache kusikiliza maneno ya mitaani badala yake waweke akilini kuwa safari imeiva na kilichobaki ni utekelezaji.
Katibu Mkuu alisema Serikali imekusudia kuhamishia Makao Makuu yake mkoani Dodoma, hivyo wizara hiyo inatekeleza maagizo hayo na inakamilisha taratibu za kuondoka.
“Suala la kuhamia Dodoma halina mahojiano tena kwa sasa, hivyo mnatakiwa kujipanga ni jinsi gani mtaishi katika mkoa huo kwani tutaondoka kwa awamu mbili tofauti na awamu ya kwanza itakuwa Novemba 30 na awamu ya pili itakuwa mwezi Juni 2017,” alisema Masima.
Aliongeza kuwa wizara hiyo itahamia Dodoma na baadhi ya Kamandi, lakini nyingine zitabaki kutokana na umuhimu wa majukumu yake kama Kamandi ya Wanamaji. Kwa upande wa Makao Makuu ya jeshi hilo, Masima
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa