Home » » HADITHI YA KUSISIMUA: KIUMBE WA USIKU SEHEMU YA 6 , TWENDE PAMOJA HAPA

HADITHI YA KUSISIMUA: KIUMBE WA USIKU SEHEMU YA 6 , TWENDE PAMOJA HAPA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Kila mmoja alikuwa na hofu yake kwa wakati huo, si unajua tena wengine walikuwa wanafunzi wa chuo, wengine ndiyo kama Suzy.

Kwa Joy hofu yake kuu ilikuwa ni kwa rafiki yake Batuli ambaye kama akigundua amekamatwa, ndiyo atapata neno la kuzungumza kuthibitisha kazi yake ya baa ni bora kuliko kujiuza, na Joy hakutaka hilo litokee.

Akatulia tuli, kiasi kwamba hata aliposimamishwa na kupakiwa ndani ya basi la magereza, akakaa zake siti ya nyuma akitafakari. 

Katika maisha yake hiyo ikiwa ni safari ya kwanza kupelekwa jela, japo kuwa alishawahi kulazwa kituo cha polisi mara nyingi sana.

Mara nyingine humalizana na polisi wanaowakamata hukohuko vijiweni mwao aidha kwa kuwapa penzi au kiasi cha pesa. Tena walifikia hatua ya kujuana na maaskari wengi sana wa vituo vya polisi, lakini mpaka kufikia wanakamatwa basi huenda ni oparesheni maalumu ya Kanda na siyo amri ya maOCD wa vituo vya polisi vidogo.

Walishinda jela siku hiyo nzima na hadi siku ya pili, wakapelekwa tena mahakamani, muda huu kesi yao ilisikilizwa mapema na wakalipa faini na kuruhusiwa kuondoka. Kila mmoja akimlaani hakimu wa mahakama wa jana yake kwa kushindwa kufika mahakamani.

Akiwa anafikiria uongo wa kumpelekea rafiki yake Batuli, akashtukia anaitwa alipogeuka alishangaa kumuona Batuli, lakini kilichomfanya kidogo azimie kwa presha, ni mtu aliyeongozana na Batuli, si mwingine bali ni yule mteja wake aliyemzima zile laki mbili siku mbili zilizopita kule, gesti huku akiviziua vitambulisho vyake nyumbani kwao.

Je, nini kitaendelea, Kwa nini Batuli alifika na yule kaka pale mahakamani, usikose kufuatilia kesho.

“Shoga pole sana, nini kimekukuta? umenipa wasiwasi kweli yaani,” alizungumza Batuli na kumkumbatia mwenzake, kama vile marafiki wakike wafanyavyo pindi wanapomisiana kwa muda mrefu.

Joy akatumia muda huo kumnong’oneza mwenzake amueleze nini kinachoendelea kati yake na yule kaka aliyongozana naye.
“Niliona kimya nikajua upo naye sehemu. Basi nikampigia simu kutumia zile namba kwenye ile kadi nikashangaa kusikia na yeye mwenyewe akasema anakutafuta kweli, ndiyo tumekuja na nilijua kama sijakukuta hapa jiji basi niende kuulizia mochwari,” alinong’ona Batuli.

Kwa jibu hilo Joy alijikuta akiishiwa nguvu akafikiria kuwa ni bora angemueleza ukweli mwenzake haya yasingetokea, lakini kwa kuwa alimficha basi hayo yalikuwa ni majuto na hana budi kuyapokea.

Akamuachia Batuli na kumfuata yule kaka aliyesimama pembeni, wakati huo akitunga uongo harakaharaka kichwani; “Mambo? Unaitwa nani vile? “ aliuliza yule jamaa huku akimtazama vizuri Joy kama vile alikuwa akiinakili sura yake ili asiisahau.

“Naitwa Joy, najua umefuata waleti yako na kweli nilitaka kukupigia sema ndiyo haya matatizo yamenikuta,” alijitetea.
“Usijali, nafahamu ugumu wa kazi yako, mimi sitaki chochote zaidi ya kile kitambulisho, ile hela unaweza ukakaa nayo tu.”
“waooh kweli?” alijikuta akishangaa Joy kwa sababu wanaume wa Kiswahili hapo ndiyo wangemuanzishia kipigo kikali na matusi huku wakitaka kila mtu ajue kuwa anamdai, lakini tofauti na yule kaka kwani alikuwa mstaarabu sana.
“Yah twendeni, nimekuja na gari,” alizungumza yule kaka akiongozana nao kutoka nje ya eneo la mahakama.

Wakapanda gari ya yule kaka na Joy akawa anaelekeza njia hadi wakafika eneo la Tandale Yemen na kupandisha mtaa wa juu hadi maeneo ya Mafioso kisha hapo wakapaki na safari ya kuelekea mabondeni mtaa wa Bitikilembwe ukaanza.

Hii kitu itaendelea usitoke hapa kuwa nasi kesho
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa