Home » » KIZIMBANI KWA KUKUTWA NA NYARA ZA SERIKALI.

KIZIMBANI KWA KUKUTWA NA NYARA ZA SERIKALI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WAKAZI wastatu wa Kijiji cha Ninde mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Nkasi katika Mkoa wa Rukwa wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Nkasi kwa kosa la kukutwa na nyara za Serikali zenye thamani ya zaidi ya Sh 900,000.

Washitakiwa hao Joseph Julio (60), Salvatory Lyambise (58) na Datus Kanondo (38), walifikishwa jana mbele ya Hakimu Lilian Lutahangwa ambako walikanusha mashtaka yao.
Awali Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi wa Polisi, Hamim Gwelo alidai mahakamani hapo kuwa watuhumiwa kwa pamoja walitenda kosa hilo Januari 30, 2016 usiku wa manane.

Kwa mujibu wa mwendesha mashtaka huyo alidai kuwa usiku huo wa tukio washtakiwa hao walikuwa wakiwa na pembe za mnyama aitwae insha na nyama ya mbawala kinyume cha sheria.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa