Home » » MKUU WA MKOA WA RUKWA ALIYEHAMISHWA KUTOKA TANGA MAGALULA SAID MAGALULA AWASILI MKOANI RUKWA NA KUKABIDHIWA RASMI OFISI YAKE MPYA

MKUU WA MKOA WA RUKWA ALIYEHAMISHWA KUTOKA TANGA MAGALULA SAID MAGALULA AWASILI MKOANI RUKWA NA KUKABIDHIWA RASMI OFISI YAKE MPYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa aliyehamishwa kutoka Tanga Mhe. Magalula Said Magalula (katikati) akisalimiana na watumishi wa ofisi yake mpya waliokusanyika kumpokea rasmi nje ya jengo la ofisi hiyo jana tarehe 22 Septemba 2015.

Mkuu Mpya wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Magalula Said Magalula kulia na Katibu Tawala Mkoa huo Ndugu Smythies Pangisa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa aliyemaliza muda wake Eng. Stella Manyanya ambaye yupo kwenye harakati za kugombea Ubunge Jimbo la Nyasa wakisaini nyaraka za makabidhiano ya ofisi mapema tarehe 22 Septemba 2015.
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa wa pili kulia kwa niaba ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo Eng. Stella Manyanya akimkabidhi rasmi nyaraka za makabidhiano ya ofisi Mkuu mpya wa Mkoa huo aliyehamishwa kutoka Tanga Mhe. Magalula Said Magalula kulia jana tarehe 22 Septemba 2015. Wanaoshuhudia kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. John Gurisha na Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu Ndugu Erasmus Rugarabamu.


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Magalula Said Magalula akizungumza muda mfupi baada ya kukabidhiwa rasmi ofisi yake mpya kufuatia uhamisho wa hivi karibuni kutoka Mkoa wa Tanga. Katika salamu zake alishukuru kwa mapokezi mazuri na kuomba ushirikiano kwa viongozi na watumishi katika kutimiza majukumu ya msingi ya kuwaletea maendeleo wananchi wa Mkoa wa Rukwa. Aliwataka viongozi pamoja na watumishi kutambua majukumu yao ya msingi ambayo ni kutoa huduma bora kwa wananchi, alisisitiza pia juu kilimo bora chenye tija kwa kuwapa wananchi huduma stahiki. Kutokana na kuwepo kwa tishio la Mvua juu wa wastani (Elnino) Mkuu huyo wa Mkoa amewaagiza viongozi wa halmashauri kuwapa wananchi wao tahadhari na kuhakikisha wanaoishi katika mazingira hatarishi wanaondoka na wengine kuboresha nyumba zao.
 Sehemu ya wakuu wa idara walioshiriki kikao hicho cha makabidhiano.
Kutoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Ndugu Methew Sedoyyeka, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Ndugu Benson Kilangi na Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Ndugu Hamid Njovu wakishuhudia makabidhiano hayo.

(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @rukwareview.blogspot.com)

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa