Home » » MAHAKAMA ZA MWANZO KANDA YA SUMBAWANGA ZAVUKA LENGO LA USIKILIZAJI WA KESI

MAHAKAMA ZA MWANZO KANDA YA SUMBAWANGA ZAVUKA LENGO LA USIKILIZAJI WA KESI


Na   Walter   Mguluchuma
Katavi
Jaji  Mfawidhi  wa  Mahakama  ya Tanzania kanda ya   Sumbawanga  Jaji  Kakusulo   Sambo  amewapongeza Mahakimu wa  Mahakama za  mwanzo    wa  Kanda ya Sumbawanga  kwa kufikia  lengo  la kutokuwa na  shauri hata moja  lenye umri wa zaidi  ya mwaka  mmoja ambalo  halijasikizwa
Pongezi hizo  alizitowa  hapo  jana  wakati alipokuwa  akifungua  kikao  cha  baraza  la wafanyakazi  wa Mahakama  ya Tanzania  Kanda ya Sumbawanga kilichofanyika  katika ukumbi wa idara ya maji Mjini Mpanda Mkoani  Katavi
Alisema     takwimu  za Mahakama   za mwanzo  zinaonyesha kuwa  kwa kanda  nzima ya Sumbawanga kwa  mwaka  wa 2014  mashauri  yote 5177  yalifunguliwa    katika   Mahakama hizo  ziliweza  kusikilizwa
  mashauri hayo  yaliokuwa  yamefunguliwa   yalipunguza   deni   ambazozilikuwa  hazijasikilizwa   mwaka 2013 kwa asilimia 2.0 sawa na mashauri  105  kati ya mashauri  1042 yaliyokuwa yamebaki mwaka 2013
  Alifafanua kuwa Mahakama imeisha weka   mwongozo  wa kila jaji  na Hakimu  kumaliza idadi  fulani  ya  mashauri  anayopaswa  kuyasikiliza  na kuyatolea  maamuzi  kwa mwaka mzima
Jaji  Sambo  alisema  kila Jaji ameishapangiwa kusikiliza  na  kumaliza    mashauri  220 Hakimu wa Wilaya na Mkoa mashauri  250 na  Hakimu wa Mahakama  ya Mwanzo  mashauri  260 kwa mwaka mzima
Alisema  ili  Mahakimu waweze kumaliza kesi   za  watu   kwa wakati ni  lazima wawajibike  na waongeze  kiwango cha uwajibikaji wa kazi yao hiyo ya uhakimu
Jaji  Sambo   alieleza kuwa  kitendo cha Mahakama   kumcheleweshea  mtu  kesi  ni  chanzo cha  kumkwamishia mtu  maendeleo yake   na  imekuwa ikiathili  jamii
Nae    Naibu  msajiri wa  wa Mahakama  kuu Sumbawanga   Romali   Mbuya  alieleza kuwa jumla ya mashauri   228  yalifunguliwa  katika  kipindi  cha mwaka 2014  katika  mahakama kuu kanda ya Sumbawanga ambapo kesi za  jinai zilikuwa   134 madai  94 na ambazo zimeishwa zikilizwa mpaka sasa ni  224 sawa na asilimia  98.2
Alisema    takwimu za  mahakama  za Wilaya  zinaonyesha   kuwa   kanda ya Sumbawanga  haina mzigo  wa mashauri  mengi  yanayopokelewa  kwa mwaka
Alifafanua kuwa ni Wilaya ya Mpanda  pekee  ndio  zipo kesi  nyingi  zilizopokelewa  kwa mwaka  ukilinganisha na Wilaya  nyingine za  kanda ya Sumbawanga  hata hivyo Mahakimu hao wameweza   kumaliza kwa kiasi kikubwa kesi hizo
 Alieleza  kwa mwaka 2014  yalifunguliwa mashauri  1545 katika   mahakama ya Wilaya ya Mpanda yenye Mahakimu watatu  na  kesi  zilizosikilizwa  zilikuwa  ni  1,601  kesi  ambazo zilikuwa zimebaki mwaka 2013  zilikuwa ni 326  kesi hizo zilisikilizwa na kuamuliwa na hakimu  mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo Chiganga   Ntengwa ambae kwa kipindi kirefu  cha mwaka jana alikuwa peke yake   kesi  zilizobaki  hadi sasa  ambazo  ni  za miaka ya nyuma ni  270  
 Alifafanua  Sumbawanga  walikuwa  na  jumla   ya  mashauri  546 kwa mwaka   kwa idadi ya  mahakimu   saba  walipo   katika  Mahakama ya Sumbawanga  ni wazi  kuwa kila Hakimu  alikuwa  na wastani  wa  mashauri  78 kwa  mwaka
Alisema  kila  hakimu  alikuwa  alikuwa na  mashauri  46 tuu kwa mwaka  mzima  kiwango hicho ni cha  chini   sana  ya kiwango  cha  kitaifa   ambacho ni mashauri 250 hii inamaana  kuwa  Mahakama ya Wilaya  ya  Sumbawanga  haikupaswa  kubaki  na shauri hata  moja  endapo  kila  hakimu  angesikiliza   mashauri 78



Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa