Home » » WATU watatu wamefariki dunia katika matukio tofauti mkoani Rukwa

WATU watatu wamefariki dunia katika matukio tofauti mkoani Rukwa


Na  Walter Mguluchuma.
Rukwa yetu
WATU watatu wamefariki dunia katika matukio tofauti mkoani Rukwa,likiwemo la mwanamke mmoja kumuua memewe kwa kupiga kichwani na mtwangio wa kinu.


Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda tukio hilo lilitokea feb 4 mwaka huu nyakati za saa asubuhi ya alfajiri baada ya kuzuka kwa ugomvi wa kifamilia baina yao.


Alisema kuwa inasemekana kwamba mwanamke huyo aitwaye Clemencia Nowa (50) kwa muda mrefu alikuwa ana maelewano na mumewe Stephen Shauri (72) hivyo asubuhi hiyo kulitokea mzozo baina yao uliosababisha kutokea kwa ugomvi mkubwa.


Ugomvi huo ulimfanya mwanamke kukimbilia mtwangio wa kinu (mchi) kisha kumpiga nao kichwani mwenza wake  hali iliyosababishia kuanguka na kufariki dunia papo hapo.


Katika tukio jingine, mkazi wa kijiji cha kipande tarafa ya kate, wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa, amefariki dunia baada ya kupigwa na radi akiwa amejificha chini ya shambani wakati mvua kubwa ikiendelea kunyesha.


Inadaiwa kuwa wakati mvua hiyo ikinyesha mwanamke huyo aitwaye Hellena Kauzeni (36) alikuwa akiendelea na shughuli zake za kilimo shambani kwake lakini ilipozidi alikwenda kujificha chini ya mti ndio radi zilizokuwa zimeambatana na mvua hiyo zipompiga na kumsababishia kifo chake.


Wakati huo huo, kijana mmoja mkazi wa katandala alifahamika kwa jina moja la utani Nokia amekutwa amefariki dunia akiwa amelala chumbani kwake, ambapo mwili huo uligundulika feb 5.


Kamanda Mwaruanda alisema kuwa kwa tukio la mwanamke kumuua mmewe tayari mwanamke huyo amekamatwa na anahojiwa tayari kwa kufikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma zinazomkabili ila kwa matukio mengine uchunguzi bado unaendelea.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa