WATU wawili
wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti mkoani Rukwa, likiwemo la
mtoto mmoja kupigwa na radi wakati akifanya shughuli za uvuvi na baba
yake mzazi.
Kwa
mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda tukio la
kijana huyo kupigwa na radi hadi kufariki lilitokea juzi nyakati za saa
moja asubuhi katika kijiji cha Kasanga mwambao wa ziwa Tanganyika na
kumtaja mtoto huyo kuwa ni Owden Sikazwe (15).
Alisema
kuwa kijana huyo akiwa na baba yake mzazi aitwaye Sikazwe Owden na mtu
mwingine aliyefahamika kuwa ni Aman Ntayanga ambapo walikuwa katika
mtumbwi wakielekea kutegua nyavu walizoweka kwa ajili ya kunasa samaki
ndipo radi hiyo hiyo ilipowatupa pembeni watu hao na kupiga kijana huyo
na kumzamisha hivyo kumsababishia kifo papo hapo.
Kamanda
Mwaruanda alisema kuwa katika tukio jingine, mwanafunzi wa mwaka wa
pili, chuo cha ualimu Rukwa Zakayo Anyosisye (25) amekutwa amefariki
dunia katika kumbi ya kuonyesha mpira kwake huko maeneo ya Chanji B
mjini hapa.
Taarifa
zinaeleza kuwa siku ya tukio nyakati za usiku baada ya watu kutazama
mpira alifunga ukumbi huo uliokuwa akiusimamia na yeye kuingia kulala
ukumbini humo.
Inasemekana
kwamba ilipofika nyakati za asubuhi, majirani walikuta mlango wa
ukumbi umevunjwa na huyo mwanafunzi akiwa humo ukumbini tayari amefariki
huku akiwa na jeraha la kupigwa na kitu kizito kichwani
Kamanda
wa Polisi Mwaruanda alisema kuwa chanzo cha mauaji hayo hakijafahamika
hadi sasa ila polisi inaendelea na uchunguzi wa tukio hilo, ili
waliohusika waweze kusakwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria ili
ichukuwe mkondo wake.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment