Walter Mguluchuma .
Sumbawanga.
HOSPITALI teule ya Dr Atman ya Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa wodi za kulaza wagonjwa kiasi cha kusababisha watoto wachanga kulazwa pamoja na watu wazima kitu ambacho ni hatari zaidi kiafya kwa watoto hao.
Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk Aaron Hyera alisema hayo jana wakati akitoa taarifa fupi ya hospitali hiyo kwa Katibu tawala wa mkoa wa Rukwa, Symthies Pangisa wakati wa hafla ya kukabidhiwa vitanda 10 na mashuka 50 kutoka mfuko wa Penisheni kwa watumishi Umma (PSPF) vyote vikiwa na thamani ya Sh milioni tano zilizofanyika katika hospitali hiyo.
Alisema kuwa hospitali hiyo ambayo ipo chini ya kanisa katoliki jimbo la Sumbawanga, inakabiliwa na changamoto hiyo hivyo baadhi ya wagonjwa ambao ni watoto wachanga na watu wazima ulazimika kulala pamoja hali ambayo ni hatari zaidi kwa watoto hao kwani kutokana na kuwa na kinga ndogo wanakuwa katika hatari kubwa ya kupata maradhi mengine kutoka kwa wagonjwa wengine.
Dk Hyera alisema kuwa katika kukabiliana na changamoto hiyo tayari uongozi wa hospitali hiyo unaendelea na ujenzi jengo la wodi ya watoto kwa fedha za mkopo kutoka Shirika la bima ya afya (NHIF) ambao waliwakopesha sh milioni 120.
Alisema licha ya kupata mkopo
huo lakini bado fedha hizo hazitoshelezi kufanikisha ukamilishaji wa
kazi hiyo, hivyo wanaendelea kuomba msaada kutoka taasisi mbalimbali
wakiwemo watu binafsi wenye moyo wa kusaidia wajitokeze kuwasaidia
baadhi ya vifaa vya kukamilisha ujenzi, vifaa tiba na madawa kwa ajili
ya wagonjwa wanaolazwa katika hospitali hiyo.Sumbawanga.
HOSPITALI teule ya Dr Atman ya Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa wodi za kulaza wagonjwa kiasi cha kusababisha watoto wachanga kulazwa pamoja na watu wazima kitu ambacho ni hatari zaidi kiafya kwa watoto hao.
Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk Aaron Hyera alisema hayo jana wakati akitoa taarifa fupi ya hospitali hiyo kwa Katibu tawala wa mkoa wa Rukwa, Symthies Pangisa wakati wa hafla ya kukabidhiwa vitanda 10 na mashuka 50 kutoka mfuko wa Penisheni kwa watumishi Umma (PSPF) vyote vikiwa na thamani ya Sh milioni tano zilizofanyika katika hospitali hiyo.
Alisema kuwa hospitali hiyo ambayo ipo chini ya kanisa katoliki jimbo la Sumbawanga, inakabiliwa na changamoto hiyo hivyo baadhi ya wagonjwa ambao ni watoto wachanga na watu wazima ulazimika kulala pamoja hali ambayo ni hatari zaidi kwa watoto hao kwani kutokana na kuwa na kinga ndogo wanakuwa katika hatari kubwa ya kupata maradhi mengine kutoka kwa wagonjwa wengine.
Dk Hyera alisema kuwa katika kukabiliana na changamoto hiyo tayari uongozi wa hospitali hiyo unaendelea na ujenzi jengo la wodi ya watoto kwa fedha za mkopo kutoka Shirika la bima ya afya (NHIF) ambao waliwakopesha sh milioni 120.
Kwa
upande wake, Katibu Tawala Pangisa licha ya kuishukuru Pspf kwa msaada
huo pia alisema kuwa umefika wakati sasa mifuko ya kijamii na makampuni
kujenga utamaduni wa kusaidia watu wenye mahitaji mbalimbali wakiwemo
watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na wagonjwa hospitalini kwani
kufanya hivyo ni sehemu ya kurudisha kile wanachopitapa kwa jamii.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
1 comments:
we jamaa date vipi man
Post a Comment