Home » » Serikali imeanzisha utaratibu wa kuvitumia vikundi vya wakulima kupitia vyama vyao vya ushirika kuvikopesha pembejeo za ruzuku kuanzia msimu ujao wa kilimo 2014/2015

Serikali imeanzisha utaratibu wa kuvitumia vikundi vya wakulima kupitia vyama vyao vya ushirika kuvikopesha pembejeo za ruzuku kuanzia msimu ujao wa kilimo 2014/2015


Na Walter Mguluchuma
Sumbawanga

Serikali  imeanzisha utaratibu wa kuvitumia vikundi vya wakulima kupitia vyama vyao vya ushirika kuvikopesha pembejeo za ruzuku kuanzia msimu ujao wa kilimo 2014/2015 kwa ajili ya wakulima katika maeneo yao  ili kukabiliana na vitendo vya udanganyifu vilivyokuwa vinafanywa na  baadhi ya watumishi wa umma wasiokuwa waaminifu katika misimu ya kilimo iliyopita

Afisa  pembejeo wa wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Gothard Lyampawe aliwaambia wakulima na wanachama wa chama cha ushirika cha msingi cha mazao na masoko kitwacho Muzia AMCOS cha mji mdogo wa Msanzi  wilayani Kalambo mkoani Rukwa wakati wa kikao cha mkutano mkuu wa chama hicho kuwa utaratibu huo utamwezesha kila mkulima kupata ruzuku stahili kwa wakati bila usumbufu

 Lyampawe aliwaambia wanachama hao na pia baadhi ya wakulima waalikwa kutoka vyama vya ushirika sita vya kata za Sopa Mkali na Matai za wilaya ya Kalambo ikiwa ni pamoja na maafisa ugani wa kata hizo na wadau wa kilimo na  mashirika yanayosambaza mbegu na mbolea mkoani Rukwa  kuwa serikali itasimamia kikamilifu utaratibu huu ili kumwezesha mkulima kulima kilimo endelevu cha faida na biashara

Alifafanua  baadhi ya wakulima wanadaiwa kukatishwa tamaa na jinsi serikali ilivyoshindwa kuthibiti ujanja wa baadhi ya wasambazaji wa ruzuku za kilimo na hivyo kulazimika kuendesha shughuli zao za kilimo kwa gharama kubwa kuliko faida wanayoipata mara baada ya mavuno yao

Nae afisa  kilimo wa wilaya ya Kalambo Nicholas Mrango ambaye katika mkutano huo alimwakilisha mrajisi wa vyama vya ushirika mkoa wa Rukwa alisema vyama vya ushirika vitakuwa na dhamana kwa wanachama wao kwa kuhakikisha pembejeo za ruzuku zinawafikia wakulima bila usumbufu kwa kuingia mikataba yenye tija kwao badala ya kuwanufaisha wafanyabiashara hao

 Alisema umeandaliwa utaratibu utakaozishirikisha bodi za vyama vya msingi vya ushirika katika kuanisha makampuni yenye sifa kwa ajili ya kuwasambazia pembejeo za kilimo kwa bei nafuu na kwa wakati ili kumnufaisha mkulima

  Wakati  wa kufungua mkutano huo mwenyekiti wa Muzia AMCOS Linus Patrick alisema mkutano huo mkuu umewashirikisha wakulima na wadau mbalimabli wa kilimo ikiwa ni wasambazaji wa mbolea  mbegu na madawa ili kushiriki kwa pamoja kutatua  changamoto zinazoukabili ushirika katika kuboresha ustawi wa wanachama

Mmoja wa  wadu wa kilimo mashirika yanayosambaza pembejeo mbalimbali za kilimo mkoani Rukwa na Katavi  Michael Rukanga wa kampuni ya mbegu ya SEEDCO  na Magnus Chaula wa kampuni ya mbolea aina ya YARA walisema wataanzisha mashamba darasa katika maeneo mbalimbali wilayani Kalambo ili kutoa elimu stahili na sahihi kwa wakulima jinsi ya kutumia mbegumbolea na madawa kwa faida ya kuongeza uzalishaji wa mazao
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa