Na Walter Mguluchuma
Sumbawanga
Kamanda wa vijana wa Chama Chama Cha
Mapinduzi –UVCCM- wilaya ya Kalambo Rosweeter Kasikila ameelezea jinsi viongozi
walioteuliwa hivi karibuni kuwa makamanda wa vijana katika ngazi za kata
wanavyotakiwa kuwa wabunifu kwa kuandaa
mazingira mazuri ya kiuchumi yatakayowezesha kuundwa kwa vikundi vya vijana vya
wajasiliamali ikiwa ni moja ya mbinu za kukabiliana na umaskini na kujiepusha
na vitendo vya uhalifu
Akizungumza na vijana wa CCM wa kata ya
Matai kwenye mji mdogo wa Matai makao makuu ya wilaya ya Kalambo baada ya
kukamilika zoezi la kuwasimika makamanda wa kata 17zinazounda tarafa 5 za
wilaya hiyo alisema makamanda hao wa kata wana wajibu wa kuwahudumia vijana
katika kata zao bila kujali itikadi zao za
vyama vya siasa na kuwahamasisha juu ya elimu ya kujitegemea
Alisema uamuzi huo wa kuwateua makamanda
hao katika ngazi za kata unalenga kukabiliana na wimbi la vijana wengi
wanaomaliza elimu katika shule za msingi na sekondari kukosa fursa ya kuendelea
na masomo ya elimu ya juu na kujikuta wanajihusisha katika vitendo mbalimbali
vya uhalifu
Kasikila ambaye pia ni mbunge wa viti
maalumu kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi mkoani Rukwa alisema changamoto
inayowakabili vijana hivi sasa ni jinsi ya kupata mitaji ya kuanzisha miradi ya
kiuchumi kutokana na kukosa umoja utakaowawezesha kuaminika na vyombo
mbalimbali vya fedha na hata halmashauri za wilaya ambazina utaratibu wa
kuvisaidia vikundi vya vijana na wanawake
Nae mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi
wilaya ya Kalambo Cledo Mpondela aliyekuwa kiongozi wa kuwasimika makamanda
hao wa kata alisema alipewa jukumu hilo la kuwapa mamlaka hayo ya kichama ili kujenga fikra za kuajiriwa miongoni mwa vijana
na kuwawezesha kujipanga kuanzisha vikundi vya ujasiliamali ambavyo itakuwa
rahisi kwao kukopesheka
Allsema makamanda hao waliosimikwa kupitia
jumuia ya vijana wa CCM watakuwa na jukumu la kusimamia mipango yote ya
maendeleo ya vijana kiuchumi na pia kushiriki katika hamasa za masuala ya kitaifa
yanayolenga kuwapiga vita maadui ujinga maradhi na umaskini licha vilevile
kujihusisha na utekelezaji wa sera za Chama Cha Mapinduzi
Mpondela alisema utaratibu huu wa kuwasimika makamanda wa vijana katika kata zote za wilaya hiyo ya Kalambo ni maagizo yanayotekelezwa katika wilaya zote za mkoa wa Rukwa na Taifa kwa ujumla kwa lengo la kusaidia kuwaunganisha vijana katika masuala yao ya kiuchumi na pia kisiasa
Aliwataka vijana wote wilayani Kalambo na
wananchi kwa ujumla kuanza kujipanga kuzitumia fursa za kimaendeleo zilizopo
hivi sasa wilayani humo ambazo ni kuanzishwa kwa wilaya mpya na ujenzi wa
barabara za lami kutoka makao makuu ya Mkoa mjini Sumbawanga kwenda bandari
ndogo ya Kasanga inayounganisha wafanyaniashara wa nchi za Tanzania na zile za
maziwa makuu za Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo Burundi na Rwanda
pia aliitaja barabara
nyingine kuwa ni ile iendayo mji wa mpakani na nchi ya Zambia wa Kasesya na pia
mradi kabambe wa usambazaji wa umeme vijijini REA ambao utavinufaisha vijiji
vingi vya wilaya hiyo na hivyo kuweka mazingira mazuri ya uzalishaji mali
kupitia vikundi vya ushirika ya kiuchumi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment