Home » » JUMUIYA YA WAZAZI RUKWA YATOA TAHADHARI

JUMUIYA YA WAZAZI RUKWA YATOA TAHADHARI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
JUMUIYA ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Rukwa, imekitaka chama hicho kuwa makini katika kutathimini uwezo na kukubalika kwao katika jamii wagombea wa nafasi mbalimbali katika chaguzi zijazo za Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Rukwa, Rainer Lukara, alisema hayo wakati akizungumza kwenye kikao cha jumuiya hiyo kilichofanyika juzi mjini hapa.
Alisema kuwa, iwapo CCM itakuwa makini katika kuwatathimini wagombea wake watakaojitokeza kuomba nafasi mbalimbali za uongozi, ni wazi haitakuwa kazi ngumu kuwanadi mbele ya jamii.
"Hatutaki kupata shida tena kama ilivyokuwa chaguzi zilizopita, kwani baadhi ya wagombea walipata upinzani mkali kutoka kwa wagombea wa vyama upinzani…..ni wakati sasa chama kuangalia sifa, uwezo, uadilifu na namna wagombea wanavyokubalika kwenye jamii," alisema Lukara.
Awali, mgeni rasmi katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Mbeya, Fatuma Katila, alionya kuhusu makundi na migawanyiko isiyo na tija na tamaa za wachache katika kutaka uongozi kwa maslahi binafsi badala ya umma.
Chanzo:Tanzania Daima 
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa