Home » » Rukwa waaswa kuchangamkia fursa ya nyumba za NHC.‏

Rukwa waaswa kuchangamkia fursa ya nyumba za NHC.‏

 Walter Mguluchuma
Sumbawanga.

UJENZI wa nyumba za kisasa unaotekelezwa na Shirika la nyumba la taifa (NHC) umetajwa kwanba ni chachu kwa halmashauri za wilaya mkoani Rukwa kutoa maeneo ya kutosha ili shirika hilo liweze kujenga nyumba ambazo zitashawishi watumishi wengi kukubali kuishi katika maeneo mengi ya mkoa huo unaokimbiwa na watumishi kwa kisingizio cha mazingira magumu ya utendaji wa kazi.

Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga, Mathew Sedoyeka alisema hayo ambaye alimwakilisha mkuu wa mkoa wa Rukwa, Stella Manyanya wakati kwenye makabidhiano ya mashine 16 za kufyatulia matofali kwa vijana zaidi ya 200 wa halmashauri zote nne za mkoa huo zilizotolewa na Shirika la nyumba la taifa katika hafla fupi iliyofanyika mjini hapa.

Sedoyeka alisema kuwa mara kadhaa watumishi wanaopangiwa kwenda Rukwa ukataa kurejea kazini mara baada ya kuripoti kwa kisingizio cha mazingira magumu ya utendaji wa kazi na ukosefu wa nyumba za kuishi hivyo sasa mpango wa ujenzi huo wa nyumba za NHC uwe chachu kwa halmashauri hizo kuchangamkia fursa hiyo kwa kutoa maeneo ya kutosha ya ujenzi wa nyumba hizo.

"Nachokiamini ni kwamba ujenzi wa nyumba hizi ukikamilika watumishi wengi watashawishika kukaa Rukwa, kisingizio cha mazingira magumu ya kazi, ukosefu wa nyumba hazitakuwepo ukizingatia kwamba pia kuna ujenzi wa barabara ya Sumbawanga hadi Tunduma kwa kiwango cha lami umekamilika" alisema Mkuu huyo wa wilaya.
Awali, Meneja wa shirika la nyumba la taifa mikoa ya Rukwa na Katavi, Nehemia Msigwa alisema kwa NHC inatekeleza miradi ya ujenzi wa nyumba bora za makazi na biashara itakayogharimu zaidi ya shilingi bilioni 8.7 kwenye manispaa ya Sumbawanga, Mpanda, Mlele na Nsimbo kwa lengo la kukabiliana na tatizo kubwa la makazi hasa kwa watumishi.
Msigwa alisema kuwa ili kufanikisha mpango huo, shirika kwa kushirikiana na wakala wa utafiti wa vifaa bora vya ujenzi wa nyumba (NHBRA) iliyo chini ya wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi, pamoja na mamlaka ya elimu na ufundi stadi (VETA) ilitoa mafunzo maalumu kwa ajili ya kujifunzia kufyatua matofali pamoja na jinsi ya kuendesha vikundi hivyo ili viwe vyenye manufaa na endelevu

Pia alitoa wito halmashauri hizo kutumia vikundi vya vijana hao kwa mahitaji ya matofali katika ujenzi mbalimbali, kwa lengo la kukuza ajira kwenye maeneo yao na kuongeza kipato kwao ikiwa ni njia mojawapo ya kuweza kuwakwamua kiuchumi na kuondoka na umasikini.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa