Home » » KIKOSI CHA ANGA NAO KUONESHA ZANA ZAO

KIKOSI CHA ANGA NAO KUONESHA ZANA ZAO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

JESHI la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Kamandi ya Anga, itafanya maadhimisho ya miaka 32 tangu kuanzishwa kwake kwa kuonesha zana za kivita zilizonunuliwa na Serikali kwa ajili ya ulinzi imara.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga nchini, Meja Jenerali Joseph Kapwani, alisema maonesho hayo yatafanyika jijini Mwanza ili kutoa fursa kwa wakazi wa mikoa ya Kanda ya Ziwa, kujionea zana za kisasa.

Alisema maadhimisho hayo yatakuwa ya kwanza kufanyika nchini tangu kuanzishwa kwa Kamandi ya Anga mwaka 1982 na yatafanyika kuanzia Julai 23 mwaka huu na kilele chake Julai 28 mwaka huu.

"Lengo la maadhimisho haya kwanza ni kusherehekea umri wa miaka 32 kwa kujitathmini kiutendaji ndani ya Kamandi, pili ni kutoa fursa kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa kuziona zana mbalimbali zilizonunuliwa na Serikali," alisema.

Alisema pamoja na jukumu la Kamandi hiyo kuhakikisha anga ya Tanzania inakuwa salama wakati wote, pia wana majukumu mengine ya ziada ambayo ni pamoja na kutoa msaada wa kimapigano kwa wanajeshi wa nchi kavu na yale ya majini.

Majukumu mengine ni kuzisaidia mamlaka za kiraia wakati wa maafa ya kitaifa, kusindikiza ndege za viongozi, kukusanya taarifa za kiusalama, kushiriki katika operesheni za kulinda amani za Umoja wa Afrika (AU), Umoja wa Mataifa (UN) na kuendeleza uhusiano wa kijeshi na nchi zingine kwa njia ya mazoezi ya pamoja.

"Kamandi hii ni miongoni mwa Kamandi tatu zinazounda JWTZ, zingine ni Kamandi ya Jeshi la Nchi kavu na Wanamaji na kila moja ina majukumu yake, kazi ya Kamandi yetu ni kulinda anga.

"Jukumu hili linatekelezwa kwa kutumia zana mbalimbali ambazo ni pamoja na ndege za kivita, usafirishaji, makombora, mizinga ya masafa marefu na mafupi ya kudungulia ndege na zana za upelelezi wa anga...katika maadhimisho haya, zana zote zitakuwepo na nyingine nyingi," alisema.

Meja Jenerali Kapwani alisema katika maonesho hayo, wananchi watapata fursa ya kuwaona marubani watatu wa ndege za kivita ambao idadi yao imeongezeka kutoka rubani mmoja.

Marubani hao wataendesha ndege za usafirishaji wa anga, upelelezi na kivita ambao kwa sasa wapo katika mazoezi kwenye nchi za China na Afrika Kusini wakiwa na elimu nzuri.

Akizungumzia mabaki ya ndege zilizoko Ukonga Dar es Salaam, Mwanza na zile za vita ya Kagera, alisema ndege hizo zitatengenezwa ili ziweze kutumika na nyingine zitabaki kama ukumbusho

Chanzo:Majira

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa