Home » » MKUU WA WILAYA YA KALAMBO, MOSHI CHAN'GA AFARIKI DUNIA

MKUU WA WILAYA YA KALAMBO, MOSHI CHAN'GA AFARIKI DUNIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, mkoani Rukwa, Moshi Chang’a enzi za uhai wake akifafanua jambo

Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, mkoani Rukwa, Moshi Chang’a amefariki dunia. Kiongozi huyo alifariki dunia jana saa 10: 15 jioni katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, alikokuwa amelazwa kwa zaidi ya siku 20.
Ofisa Habari wa hospitali hiyo, Aminieli Aligaesha alisema DC Chang’a alifika hospitalini hapo Machi 29, mwaka huu akiwa anaumwa na kulazwa.
Alisema madaktari wamekuwa wakimpatia matibabu, lakini ilipofika jana saa 9:30 alasiri hali yake ilibadilika ghafla.
“Walijitahidi kuokoa uhai wake bila mafanikio na ilipofika saa 10: 15 alikata roho, alisema Aligaesha huku akikataa kueleza tatizo lililokuwa linamsibu.
“Huyu ni kiongozi wa Serikali, bila shaka wakubwa huko serikalini wataeleza zaidi kuhusu kifo hicho,” alisema.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Hawa Ghasia alithibitisha kutokea kwa kifo hicho mchana wa jana, baada ya kiongozi huyo kusumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu.
Alisema amemwagiza katibu wake (wa waziri) na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Stella Manyanya kufuatilia na kushughulikia msiba huo na taarifa zaidi kuhusu utaratibu zitapatikana leo baada ya kuzungumza na familia.
Chang’a kabla ya kuhamishiwa katika Wilaya ya Kalambo alikuwa DC wa Wilaya Mpya ya Mkalama.
Chanzo;Mwananchi
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa