Home » » MKUU WA MKOA WA RUKWA ASHIRIKI NA UVCCM KATIKA MBIO ZA UZALENDO TANZANIA KUADHIMISHA MIAKA 50 YA MUUNGANO WA TANZANIA

MKUU WA MKOA WA RUKWA ASHIRIKI NA UVCCM KATIKA MBIO ZA UZALENDO TANZANIA KUADHIMISHA MIAKA 50 YA MUUNGANO WA TANZANIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akipokea msafara wa pikipiki wa vijana wa CCM (UVCCM) ambao wanaendesha mbio za Uzalendo Tanzania zikiwa na lengo la kuadhimisha Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar jana tarehe 07-04-2014. Mbio hizo za kitaifa zinahusisha msafara wa pikipiki tano zinazoongozwa na viongozi watatu wa UVCCM ambao wanakuwa kwenye gari, aidha zinashirikisha wadau mbalimbali wa UVCCM katika kuzifanikisha. Mbio hizo  zinahimiza vijana kudumisha muungano, kuweka utaifa mbele na kutumia fursa zilizopo kwa maendeleo yao. Mbio hizo zitakuwa Mkoani Rukwa tarehe 07 na 08 April 2014 na kuelekea Mkoani Mbeya. 
Ujumbe wa mbio hizo za Uzalendo Tanzania ambazo zinaendeshwa na UVCCM.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya (kati) akiendesha duwa rasmi ya kuwaombea viongozi waasisi wa Muungano ambao wametangulia mbele za haki kama wanavyonekana kwenye picha Hayati Mwalim Julius K. Nyerere na Hayati Abeid Amani Karume muda mfupi baada ya kupokea msafara wa mbio hizi ofisini kwake jana tarehe 07-04-2014.
Msafara wa Mbio za Uzalendo Tanzania ukiondoka katika Ofisi ya Mkuu ya Mkoa wa Rukwa mara baada ya kupata baraka za kiongozi huyo na kusaini kitabu tayari kwa zoezi la mbio hizo katika Manispaa ya Sumbawanga na baadae kuelekea katika Mji Mdogo wa Laela.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akiondoka na pikipiki iliyokuwa ikiendeshwa na Katibu wa UVCCM Mkoa wa Rukwa Ndugu Philipo Elieza ambapo alishiriki mbio hizo hadi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika nje ya uwanja wa Nelson Mandela katikati ya Manispaa ya Sumbawanga.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akiongoza mbio hizo na vijana wa UVCCM kuelekea kwenye mkutano wa hadhara.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya (Mb) akizungumza katika Mkutano wa hadhara ambapo alisema tunu ya muungano ni lazma ilindwe na kila moja wetu na kuwa sio jambo la hiari. Aliongeza kuwa madai ya uwepo wa Serikali tatu ni hatua za kuhatarisha Muungano uliopo wa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar hivyo hakuna budi kuimarisha Muungano wa Serikali mbili kwa maslahi watanzania wote. Aliuotelea mfano muungano wa Serikali tatu kuwa hauna tofauti na kuchukua kisu na kugawana mtoto ambapo kila mzazi atachukua kipande ambacho sio mtoto kamili.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa akizungumza kwenye mkutano wa hadhara.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akimkabidhi Katibu wa UVCCM Mkoa wa Rukwa Ndugu Philipo Elieza cheti cha pongezi kwa ushiriki wa Mbio za Uzalendo Tanzania na kingine kwa UVCCM Mkoa na Taifa kwa kuandaa na kufanikisha mbio hizo. Mkuu huyo wa Mkoa aliandaa vyeti vya pongezi kwa washiriki wote wa mbio hizo.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Rukwa Ndugu Agustino Mzurikwao akitoa salam za vijana wa CCM katika mkutano huo wa hadhara ambapo alisisitiza juu ya vijana kutumia fursa zilizopo katika kujiendeleza kiuchumi na kudumisha Muungano wa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar. Kulia ni Katibu Muenezi wa CCM Mkoa wa Rukwa Ndugu Clemence Bakuli.
(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa