Home » » Kifo cha DC: Rais Kikwete amtumia salamu Waziri Mkuu

Kifo cha DC: Rais Kikwete amtumia salamu Waziri Mkuu

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

IMG_3959
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda kuomboleza kifo cha Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Mkoa wa Rukwa, Ndugu Moshi Chang’a(pichani).
“Ni kifo cha kusikitisha kwa sababu kimepunguza safu ya uongozi wetu na kimelinyang’anya taifa letu mhamasishaji hodari na mtetezi wa kuaminika wa maendeleo ya wananchi,” Rais Kikwete amesema katika salamu hizo.
Amesema Rais Kikwete katika salamu zake za rambirambi: “Nilimjua Ndugu Chang’a kwa miaka mingi tokea mwaka 1979 alipojiunga na utumishi wa Chama cha Mapinduzi ambacho pia alikitumia kwa uaminifu mkubwa hadi alipoteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya mwaka 2003. Alikuwa kiongozi wa kweli kweli wa maendeleo na kifo chake kimetuachia pengo la uongozi.”
“Nakutumia salamu zangu za dhati kuomboleza msiba huu. Aidha, kupitia kwako, naitumia familia wa Ndugu Chang’a pole za dhati ya moyo wangu kwa kuondokewa na mzazi na mhimili wa familia. Nakuomba uwajulishe kuwa naelewa machungu yao katika kipindi hiki na nawaombea subira na uvumilivu kwa sababu yote ni mapenzi ya Mungu. Aidha, naungana nao katika kumwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, aiweke peponi roho ya marehemu. Amen,” amesema Rais katika salamu hizo.
Ndugu Moshi Chang’a ambaye aliaga dunia jioni ya, Jumapili, Aprili 20, 2014  katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili, Dar Es Salaam amekuwa mkuu wa wilaya katika Mikoa ya Mbeya, Tabora na Rukwa.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa