Home » » CCM:TUTAREJESHA MAJIMBO YOTE YA UPINZANI

CCM:TUTAREJESHA MAJIMBO YOTE YA UPINZANI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema hivi sasa kipo makini kuhakikisha kinaweka udhibiti wa kutosha wa makundi majimboni. Pia chama hicho, kimesisitiza kuwa, kutokana na kukithiri kwa makundi hayo, viongozi wake wa kitaifa wamekuwa hawalali kwa kuangalia namna ya kurejesha majimbo yote ya wapinzani mikononi mwa chama hicho.
Hayo yalisema mwishoni mwa wiki na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, alipozungumza kwa nyakati tofauti na wajumbe wa Halmashauri Kuu za Wilaya ya Nkasi, Kalambo na Sumbawanga ambako amehitimisha ziara yake ya kukagua Ilani na kuimarisha chama hicho, mkoani Rukwa.
Akizungumza na wajumbe wa halmashauri hizo, Kinana aliweka msisitizo na kuwataka wana CCM nchini kote kuhakikisha wanakuwa kitu kimoja na kuepuka makundi ya uchaguzi.
Alisema umoja ndio ushindi na iwapo kila mwanachama wa chama hicho, atalitambua hilo na kulitekeleza kwa vitendo, chama hicho katika uchaguzi ujao, kitakuwa salama na kuibuka na ushindi wa kishindo.
"Kutokana na hali hii, Kamati Kuu na NEC ipo macho kuhakikisha tunarejesha majimbo yote yaliyokuwa katika mikono ya wapinzani, na nikiwa kama mtendaji wa chama ninazo taarifa za kuanza kwa vurugu hasa katika majimbo yanaongozwa na wapinzani," alisema Kinana.
Alisema iwapo wanachama wa chama hicho watashindwa kushikamana na hata kuwa na mipango ni wazi kuwa chama hicho kitashindwa kuyarejesha majimbo hayo.
"Hili siko tayari kuliona na kila mwana CCM atambue hivyo." Kinana alisema kutokana na hali hiyo, wananchi wengi walikata tamaa na kutafuta njia mbadala na kuunga mkono upinzani.
"Najua wengi walichagua upinzani kutokana na kukata tamaa, hili tulibadilishe, tuwajibike."
Chanzo;Habari Leo
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa